Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2020

UONGOZI WA JUU WA CHADEMA UNAHUSIKA MOJA KWA MOJA NA UTEUZI WA WABUNGE WA VITI MAALUM WALIO APA TAREHE 24/11/2020

Picha
  Tarehe 25/11/2020 Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika aliongea na waandishi wa habari mambo mengi yakujibaraguza kuhusu wabunge wa viti maalum walioapishwa siku ya tarehe 24.11.2020 na Mhe. Spika Job Ndugai Jijini Dodoma. Kama ulipata bahati ya kumsikiliza Mnyika vizuri basi utaelewa kuwa CHADEMA wanawachezea mchezo wa mind-game wafuasi wao kuwa hawahusiki na tukio hilo la kuteua wabunge hao wakati hali halisi ni kuwa wanahusika kwa asilimia zote. Mambo haya ni uthibitisho  kuwa CHADEMA inahusika moja kwa moja na uteuzi wa wabunge hao:- 1. Kamati kuu ya CHADEMA ingekutana kwa dharura tangu jana (hata kwa kufanya online meeting kama walivyowai kufanya kipindi kile walivyokimbia vikao vya bungeni kwa kudai kuwa wanajilinda na COVID-19) na leo wangekuja na jibu la moja kwa moja kuhusu wabunge hao kwasababu ni tukio kubwa mno ndani ya chama hicho. 2. Tutaaminije kama tukio hilo halina Baraka kutoka  uongozi wa juu wa chama, makaratasi aliyoyaonesha Mnyika eti hajayajaza what if ni cop

HONGERA HALIMA MDEE NA WENZAKO KWA KUFUNGUA MINYORORO YA MFUMO DUME NA UBINAFSI NDANI YA CHADEMA

Picha
Kila Novemba 25 ulimwengu huaadhimisha Siku ya Kupambana na Ukatili Dhidi ya Wanawake, mwaka huu wa 2020 kauli mbiu inasema ''Ipake Dunia Rangi ya Chungwa: Nisikie Nami Pia. Kupinga Ukatili wa Kijinsia, Inaanza na Mimi.'' Maadhimisho ya siku hiyo nchini mwaka huu yamepambwa na tukio la kishujaa lililofanywa na Wanachama wa Bawacha wapatao 19 wakioongozwa na Mwenyekiti Taifa wa baraza hilo Halima Mdee walioamua kukataa ukatili dhidi yao wa kukatazwa na Uongozi wa CHADEMA wasiwakilishe jamii kubwa ya wanawake katika chombo muhimu cha kufanya maamuzi cha Bunge. Kwa nini Taifa zima limewapongeza wabunge wa viti maalum wa Chadema kwa uamuzi huo? kwa Sababu haikuwa rahisi kwao kuvuka vikwazo vya mfumo dume na imani kwamba “wanaume wana sauti ya Mwisho kwenye maamuzi” hata ya wao kwenda kuapa kuwa wabunge licha ya kuwa ni haki yao kikatiba. Viongozi wa Kitaifa wa CHADEMA (Wanaume) ni wabinafsi wanaojali maslahi yao, kwa sababu wao wanaendelea kuneemeka na fedha kutoka kwa mata

TUNDU LISSU ULIKUWA UNATUDANGANYA!!

Na WanaCHADEMA Kanda ya Kaskazini Yuko wapi Tundu Lissu ambaye alituhamasisha wananchama wa CHADEMA kuandamana nchi nzima kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu, hayupo nchini ameondoka kwenda Ubelgiji huku akisindikizwa na maafisa wa Ubalozi wa Ujerumani mpaka uwanja wa ndege!!! Hapa ndipo tunapogundua kuwa Tundu Lissu hakuwa pamoja nasi bali alikuwa anatudanganya kwa kutushawishi tuingie barabarani kuandamana na kufanya vurugu ilhali akijua kwa upande wake haitamletea matatizo kwa kuwa alishaandaliwa mpango na Mataifa ya Magharibi kuondolewa nchini baada ya kusababisha vurugu na machafuko nchini.  Sasa tunajiuliza endapo tungeingia barabarani kuandamana tungekuwa katika hali gani? Maana aliyekuwa anahamasisha maandamano angekuwa katika mazingira salama na kutuacha sisi tukiwa katika hali mbaya baada ya kusababisha vurugu nchini, tungekosa mahali pa kwenda, kwani wote walikuwa wanaunga mkono maandamano wameshapata mahali pa kujihifadhi, Tundu Lissu nchini Ubelgiji, Godbless Lema nchini Keny

TUNDU LISSU ALIVYOIGHARIMU CHADEMA KISIASA NA KIUCHUMI KUELEKEA 2025

 Kwanza kabisa mtakumbuka kipindi ambapo Zitto Kabwe alimshawishi Tundu Lissu kujiunga na chama cha ACT Wazalendo kwa kumuahidi kumpendekezwa kuwa mgombea Urais kupitia chama hicho, jambo ambalo Mbowe alilitambua mapema  na kuamua kumpa cheo cha Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, hivyo Lissu akashindwa kutimkia ACT Wazalendo na kuamua kuukwaa Umakamu Mwenyekiti wa CHADEMA baada ya kuahidiwa kuwa mgombea Urais 2020. Baada ya CHADEMA kumpa Lissu nafasi ya kugombea Urais kupitia chama hicho ndipo walipojipalia makaa ya moto vichwani mwao na hawakutegemea kuona mambo ambayo aliyafanya majukwaani wakati wa kampeni za uchaguzi, tuanze na kuyaangazia haya:- ● Kwanza kabisa alifanya siasa za kujielezea yeye binafsi majukwaani hasa tukio lake la kupigwa risasi. Siku ya ufunguzi wa kampeni Lissu hakuongea kabisa sera za chama hicho bali alijikita kuelezea matatizo yake binafsi mpaka ikabidi siku ya pili ya kampeni Mbowe kumwomba ajikite kuelezea sera na sio mambo binafsi ila Lissu hakufanya hivyo,

MPANGO WA MAANDAMANO YANAYORATIBIWA NA CHAMA CHA ACT WAZALENDO NA CHADEMA WAVUJA.

Raia Mwema. Jioni hii baadhi ya viongozi wa CHADEMA kutoka mikoa tofauti, wamewasili Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya maandamano siku ya Tarehe 02/11/2020. Lengo lao ni "kulianzisha" hapa Dar es Salaam ndipo baadae isambae mikoani. Mambo yaliyopangwa ni pamoja na kuchoma Matairi barabarani na kuleta vurugu za aina nyingi ili shughuli za kijamii zisimame. Wamepanga mambo haya yaanze asubuhi ya siku ya Tarehe 02/11/2020 kwakuwa siku hiyo ni siku ya Kazi, hivyo lengo  ni kufanya watu washindwe kwenda Makazini. Pia  vijana maalumu wataanzisha vurugu kwa ajili ya kufanya "looting" Kwenye sehemu za biashara.  CHADEMA imegawagawa makundi Tofauti na haswa wamelenga Barabara zinazo ingia mjini, barabara inayo toka Kimara kuna vituo wameviweka na wata ziba kabisa njia. Pia Barabara za Mbagala, Tegeta  na Barabara ya Banana (njia zote hizi zipo kwenye mpango wa kufungwa kabisa). Aidha ,  kuna kundi moja la ACT WAZALENDO ambalo zamani walikuwa CUF na lipo maeneo ya Bug

WALIOKUWA WANATUMIWA NA MABEBERU KUICHAFUA TANZANIA WAANZA KUTOROKA NCHINI

Picha
Habari za muda huu wanafuatiliaji na wachambuzi wa masuala ya kisiasa hapa Nchini. Kwa miaka kadhaa sasa kumekuwa na fununu na minong’ono ya chini chini kuwa baadhi ya wanasiasa wanatumiwa na Mataifa ya Nje kuishawishi na kuishinikiza Serikali kupitisha ama kutunga sera ambazo zinaweza kuyanufaisha Mataifa hayo huku wao wakipewa fedha pamoja na kuahidiwa hifadhi iwapo njama zao zitabainika na Serikali. Tulishuhudia kipindi cha Makinikia baadhi ya wanasiasa hao akiwemo aliyekwa mgombea wa Urais kupitia CHADEMA Tundu Lissu walisimama kidete kuwatetea wanyonyaji wa rasilimali za Nchi yetu huku wakitishia kuwa Serikali itafunguliwa mashitaka kwa kitendo hicho cha kuzuia makinikia, na walifanya hivyo makusudi kwa kupewa maelekezo hayo na Mataifa hayo ili Serikali isiendelee kuzuia makinikia hayo. Baadhi ya wanasiasa akiwemo Zitto Kabwe walioandika mpaka barua kwenye Taasisi za kifedha Duniani ili Tanzania inyimwe mikopo ya kuboresha Sekta ya Elimu Nchini, wengine walizunguka kwenye Mataifa