Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2021

WALICHOSEMA TEC NI USHAURI KAMA WALIVYOFANYA MWAKA 2020. TUSIPOTOSHE

Vyombo vya ndani na nje vimekuwa mstari wa mbele kupotosha waraka uliotolewa na Baraza la Maaskofu Tanzania ( TEC) kuhusu kujilinda na virusi vipya vinavyosababisha virusi vya corona vilivyogunduliwa Afrika ya Kusini na Uingereza. Wakati Baraza la Maaskofu likiwaomba watanzania kuchukua tahadhali kwa kuwa Tanzania sio kisiwa, vyombo vya habari vimesema Baraza limesema Tanzania kuna virusi hivyo vipya. Ukweli ni kwamba ukisoma waraka huo hauna tofauti kubwa na ule walioutoa mwaka 2020 mwezi wa pili ukiwaomba watanzania kuchukua tahadhali. Ikumbukwe kuwa dini na viongozi wote wa imani wanalo jukumu la kuwakumbusha waumini kutenda na kuishi maisha mema. Hili ndo walilofanya Baraza la Maaskofu kuwakumbusha waamini wao na watanzania kwa ujumla kutokubweteka na kuendelea kufuata miongozo iliyotolewa na wizara ya afya ya kunawa mikono, kuvaa barakoa, kuepuka misongamano isiyo ya lazima na mingine mingi. Ni kwa msingi huo ukisoma waraka huo hakuna popote unaposema Tanzania kuna virusi vipya vi

Barua ya Wazi kwa Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula

Picha
Amani iwe kwako! Mimi nikiwa kama muumini wa Kanisa lako la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki nimeshangazwa na ujumbe ulioutuma katika barua ya wazi kwa Mhe.Rais Dkt John Pombe Magufuli kwani umeacha jukumu la msingi uliloitiwa na Mungu la kutuhubiria wananchi ili tuokoke na kumrudia Mungu. Inafikirisha kukuona Askofu wangu ukiacha majukumu yako na kuanza kufanya siasa, najiuliza huo wito aliopewa na Mungu ni kwa ajili ya kuhubiri neno au kufanya siasa? Nawaomba Mhe.Rais Magufuli pamoja na washauri wake na Watanzania kwa ujumla wenu muupuuze ujumbe huo  alioutoa kwani hauna nia njema ya kutujenga Wananchi zaidi ya kutugawa. Askofu wangu Mwamakula  umesema kuwa unataka kufanya "Matembezi ya Hiyari" nchi nzima yenye lengo la kuuhamasisha Umma wa Tanzania kuhusu Kuunda Tume Huru ya Uchaguzi na Kuandika Katiba Mpya. Najiuliza tu hivi nilishawahi kukusikia au kukuona ukifanya  matembezi ya hiyari kuhamasisha watu kumjua Mungu na kuokoka? Jibu ni hapana!.  Kwanini