Aliyegombea Ubunge Jimbo la Siha kupitia Chadema Elvis Christopher Mosi Atimukia CCM
Wakati Tukielekea Kuupokea Mwaka 2021 Leo Aliyekuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Siha Kwa Tiketi Ya Chadema Kamanda ELVIS CHRISTOPHER MOSI Leo Amemwaga Manyanga na Kujiunga Na Chama Cha Mapinduzi. Aidha, Ndugu ELVIS CHRISTOPHER MOSI Ameamua Kujiunga na Chama Cha Mapinduzi Kutokana na Sera za Chama Cha Mapinduzi Zilizojikita Katika Kuleta Maendeleo Kwa WaTanzania. Sambamba na Zoezi Hilo Pia Aliyekuwa Katibu Wa Chadema Wilaya ya Siha na Mjumbe wa Baraza Kuu Chadema Taifa Kamanda Emanuel Nabora Amestaafu Siasa na Kuachana Na Nafasi Zake Zote Ndani Ya Chadema.