Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2020

UJASUSI WA MEMBE WAUANGUSHA UPINZANI

Picha
  LAZIMA tujue kuwa anguko la CHADEMA mwaka huu ni la kihistoria. Haijawahi kutokea tangu kuanza kwa Mfumo wa Vyama vingi mwaka 1992. Labda kwa wasiofahamu dhambi ya kumkataa Jasusi au Kachero (Membe) kwenye Chama hicho ndio mwanzo wa kujiangusha wenyewe. Membe hakuridhika kukataliwa na CHADEMA akaamua kwenda ACT - Wazalendo ili iwe route ya kuwavuruga wote wawili. Ubaya ulianzia wapi? Baada tu ya mazungumzo na Viongozi waandamizi wa CHADEMA na Membe kutokubaliana kwa kuwa Membe alionesha kuwa anakwenda kwenye Chama na CASH za kutosha lakini Viongozi hao waliona ni bora aliyepigwa risasi (Lissu) kwa kuwa wananchi watamuonea huruma. Alichofanya Membe baada ya kutemwa CHADEMA Kwa kuwa Membe alikosa njia ya kuingia na kuibomoa CHADEMA aliamua kujiunga na ACT Wazalendo ili kuwapasua vizuri wote wawili kwa pamoja na lengo la kwanza likatimia. CHADEMA na ACT Wazalendo walijikanyaga wapi? Siku ambayo Mgombea wa Urais wa CHADEMA Lissu alipoenda kwenye Mkutano Mkuu wa ACT Wazalendo na kuhutubia

WATUMIAJI WA MTANDAO WA INTANETI TANZANIA WAMTABIRIA MAGUFULI USHINDI

Picha
Sagati Chacha Huku zikiwa zimesalia siku mbili Watanzania kupiga kura za kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani, baadhi ya Watanzania wanaotumia mtandao wa intaneti wamemtabiria ushindi Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt John Pombe Magufuli, na hii ni kwa mujibu wa kura ya maoni inayoendeshwa na tovuti maarufu ya kurayamtandaoni.com. Takwimu za tovuti hiyo zinaonyesha kuwa, mpaka kufikia alasiri ya leo Oktoba 26, jumla ya watu 28,304 walikuwa tayari wamepiga kura ya maoni katika mtandao huo, huku Dkt Magufuli akipata kura 20,359 sawa na asilimia 72.9, akifuatiwa na Mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu mwenye kura 5,294, sawa na asilimia 18.7.  Oktoba 28 mwaka huu, Tanzania itafanya Uchaguzi Mkuu wa 6 wa vyama vingi, tangu kuanza kwa mfumo huo mwezi Julai mwaka 1992. Mvutano mkubwa katika uchaguzi wa mwaka huu unatarajiwa kuwa kati ya vyama vya CCM na CHADEMA. Dkt John Magufuli anagombea muhula wa pili, akijinadi kwa kazi ya miaka mitano ya awali katika kuboresha miundombinu, upatikanaji wa ume

MTEGO WA ZITTO KABWE WAINASA CHADEMA DAKIKA ZA MWISHO

Picha
Habari wafuatiliaji na wapenzi wa siasa za Tanzania. Leo tutaanzia nyuma kidogo mwaka 2013 kipindi ambacho Zitto Kabwe alijiengua wadhifa wake wa  Unaibu Katibu Mkuu wa Chama cha Deokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kueleza kuwa yeye hatojitoa CHADEMA kwa ridhaa yake ila kama CHADEMA wataamua kumfukuza basi ataondoka. Kipindi hicho kulikuwa na minong’ono mingi kumuhusu Zitto Kabwe kwamba ni msalti wa chama chao, mara anatumiwa na CCM kuihujumu CHADEMA mara wengine wakamtetea na kueleza kuwa ni njia za kumdhibiti ili asigombee nafasi ya uenyekiti wa chama hicho. Anyway, CHADEMA na Zitto Kabwe wanaelewa undani na ukweli wa mambo hayo. Baada ya purukushani hizo zote, zilisababisha Zitto Kabwe kuanzisha chama chake cha ACT Wazalendo, ambapo nadhani ilikuwa ni smart move kwake.  Hivi karibuni wakati wa mchakato huu wa kuelekea Uchaguzi Mkuu tulisikia tetesi nyingi kuhusu Vyama vya upinzani kuungana ili kumsimamisha mgombea mmoja wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuachi

KISHERIA ACT HAINA MGOMBEA URAIS ZANZIBAR WALA ZITO SI MBUNGE WA ACT TENA

Picha
 Na Mwamba wa Kaskazini Jamaa mmoja aliwahi kuniambia sikia tu kitu inaitwa utawala bora au imba sana kuhusu hiyo kitu lakini ukiwa wewe ndio unatakiwa kutekeleza hapo kwa wengi vumbi kubwa hutimka. Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe na Mgombea wake huko Zanzibar Maalim Seif Sharrif Hamad wamekosa sifa za kuendelea kuongoza na hata kuwa wagombea wa chama hicho. Hii inakuja kufuatia Ibara ya 11(4) ya Katiba ya Chama hicho Toleo la 2015 kusisitiza wazi kuwa mtu atakoma kuwa mwanachama wa ACT Wazalendo iwapo atatangaza kuunga mkono mgombea wa Chama kingine wakati chama hicho kimeweka mgombea. Kwa kauli hii ya Katiba na kitendo cha sasa cha Zitto na Maalim Seif kutangaza hadharani kuwa wanamuunga mkono mgombea wa CHADEMA wa Urais, Tundu Lissu, wakati Chama hicho cha ACT bado kina mgombea wake wa Urais, Ndugu Bernard Membe.  Kwa Katiba hiyo Maalim Seif amekoma kuwa mwanachama wa ACT na hivyo anakosa sifa za kugombea Urais wa Zanzibar. Zitto pia anaanguka kuwa mwanachama w

Hoja Tano Za Muungano Zapatiwa Ufumbuzi

Picha
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), zimetia saini hati za makubaliano kuondoa hoja za Muungano zilizopatiwa ufumbuzi ambazo ni ushirikishwaji wa SMZ kwenye masuala ya kimataifa na kikanda, Ushiriki wa Zanzibar katika jumuiya ya Afrika Mashariki, gharama za kushusha mizigo bandari ya Dar es Salaam kwa mizigo inayotoka Zanzibar, utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi pamoja na utaratibu wa vikao vya kamati ya pamoja ya SMT na SMZ ya kushughulikia masuala ya Muungano. Hafla hiyo imefanyika leo tarehe 17 Oktoba, 2020 katika ukumbi wa mikutano Ikulu- Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali waserikali akiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi na Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mgombea urais wa Zanzibar, Dkt.Hussein Mwinyi pamoja na Wanasheria Wakuu wa Ser

LISSU USIPOTOSHE, UJENZI WA UWANJA WA NGEDE CHATO NI MUHIMU KWA TAIFA

Picha
Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu kampeni za Urais zinazoendelea Nchini, jana nilimsikia mgombea wa Urais wa CHADEMA TUNDU LISSU akijinadi kwa kubeza jitihada zilizofanywa na Serikali katika kujenga Uwanja wa Ndege wa Chato, Mkoani Geita. Kabla ya Kuanza kujadili kwa kina kuhusu tija ya uwanja huo, ni AIBU kwa mgombea wa nafasi ya Urais kubeza suala la ujenzi wa kiwanja cha Ndege na kuifanya kuwa ajenda kuu ya kumuingiza Ikulu, katika hali ya kawaida tulitarajia mgombea wa nafasi ya Urais wa upinzani kuja na Sera mbadala kabambe na madhubuti za kiuchumi, kisiasa na kijamii ili kuvuta hisia za wapiga kura. Turejee kwenye mjadala wetu mama wa ujenzi wa uwanja wa Ndege Chato, nilichobaini katika mijadala mingi inayoendelea kuhusu jambo hilo ni wachangiaji wengi wanaongozwa na mihemko na itikadi za kisiasa bila kuwa na tafakuri ya kina ili kubaini uhalisia wa jambo hilo. Ili kuwa na uelewa  wa pamoja, kwa nini ujenzi huo ulifanyika Chato ni muhimu tukafahamu mambo  machache kuhusu Chato, G

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TAARIFA ILIYOTOLEWA NA AMNESTY INTERNATIONAL

Picha
  Tarehe 12/10/2020 Shirika la AMNESTY INTERNATIONAL lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari iliyojaa upotoshaji kuhusu Serikali ya Tanzania, kwamba inakandamiza ASASI za kiraia kwa kuziwekea utaratibu wa usajili, kuwachukuliwa hatua wanasiasa wa upinzani wanaovunja sheria za nchi kwa makusudi pamoja na wanaharakati wa mitandaoni. Katika ripoti yao wamelenga kutetea baadhi ya makundi yanayohamasisha uvunjifu wa amani nchini pamoja na kueneza agenda ya mapenzi ya jinsia moja (ushoga). Shirika hili ni moja ya Mashirika yanayotumiwa na mabeberu kuishambulia Serikali ya Tanzania na  Mhe. Rais Dkt.  John Pombe Magufuli. Katika Ripoti hiyo Amnesty imepotosha katika mambo yafuatayo:- 1. Ripoti hiyo imetetea watumiaji wa mitandao ya kijamii hasa wale wanaotukana  na kuwakejeli viongozi wa Serikali pamoja na viongozi wa dini wanao kemea unyonyaji wa rasilimali za nchi na  kwa kiasi kikubwa ripoti hiyo imewatetea wanaohamasisha ushoga kwa kueleza kuwa kila mtu ana uhuru wa kueleza hisia zake bil

BE AWARE, Robert Amsterdam is a Canadian Set to Plant Violence in African Countries.

Picha
I am writing this article as an African. Diaspora alerting the African Union to be aware with Robert Amsterdam who claims to be  an international lawyer and Political Adviser. Amsterdam has started to set a violence strategy in African countries heading to their elections. Mr. Amsterdam is famous to us as the Canadian International lawyer who was born in 1956.  He runs the law firm called Amsterdam& Partners, with offices  in. Washington D.C. and London. Credible investigators information confirmed that for a cup of years Amsterdam has supported political violence in Europe, Asia, Latin America, Middle East and  Africa. Amsterdam who was awarded a BA from Carleton University ( Ottawa, Canada)  in 1975 and LLB from Queen's University ( Kingston, Canada) in 1978 is practicing  Public International law, international criminal law and political advocacy as well as  providing  dangerous directives to institutions and persons with political risk guidance. He is Proffesional on issues

SIKU YA WAZEE DUNIANI, UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KWA WAZEE

Picha
Tukiwa tunaadhimisha Siku ya Wazee Duniani ni vyema tukakumbushana juu ya Sera ya Taifa kwa Wazee. Yaliyotekelezwa kwa Wazee Mwaka 2015 - 2020 Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Chama Cha Mapinduzi kiliendelea kuisimamia Serikali kutekeleza Sera ya Taifa ya Wazee ambapo mafanikio yafuatayo yamepatikana:-  (a) Kuongezeka kwa idadi ya wazee waliopatiwa vitambulisho vya kuwawezesha kupata matibabu bila malipo kutoka 213,025 mwaka 2015 hadi kufikia wazee 1,042,403 mwaka 2020. (b) Wazee na wasiojiweza 2,135 wanaoishi katika makazi 16 yanayomilikiwa na Serikali walipatiwa huduma za msingi za chakula, malazi, mavazi na matibabu kati ya mwaka 2015 na 2020. (c) Kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya kwa Wazee kwa kuanzisha madirisha 2,335 ya kutolea huduma za afya kwa wazee katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini. (d) Kuanzishwa kwa mabaraza ya wazee 8,183 ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa haki kwa wazee. (e) Kudhibiti mauaji ya wazee kwa kutekeleza Mkakati wa Kutokomeza Maua