Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2021

CHADEMA Yalalamikiwa kupoteza Mvuto wa Kisiasa

Picha
''Mimi ni Mtanzania ninaishi nchini Marekani katika mji wa Chicago kiitikadi ni mfuasi wa CHADEMA, nimeguswa kuandika Makala hii kueleza masikitiko niliyonayo kwa vyama vya upinzani nchini hususani chama changu. Nianze na kusema kuwa CHADEMA kilikuwa ni chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania hakikuwa na mpinzani kilijikita kuikosoa Serikali na kutoa mawazo mbadala, kwa sasa hali imekuwa ya tofauti kwani CHADEMA wameshindwa kutimiza wajibu wao wa kukosoa na kutoa mawazo mbadala. CHADEMA kwa sasa hawana agenda wamebakia kudandia agenda za Serikali na chama Tawala CCM, yani nimekuwa nikifuatilia hawana wanachokifanya wamebakia tu kulalamikia mambo mbalimbali yanayofanywa na Serikali bila kutoa ushauri wa nini kifanyike. Naumia sana kuona chama changu kikishindwa kusimama katika nafasi yake, mpaka vyama vya wasaliti vilivyoanza juzi tu vinaanza kuleta upinzani. Najiuliza tatizo nini? Je ni mfumo wa uongozi? Je viongozi kutojua majukumu yao?  Hivi karibuni nimeshuhudia wanachadema

Manufaa ya Ushirikiano wa Tanzania na Kenya

Picha
  Tanzania na Kenya zimekubaliana kushirikiana kuondoa vikwazo vya biashara na kufungua milango Zaidi ya kuwekeza na kuinua uchumi baina ya nchi zote mbili. Makubaliano hayo yamefikiwa kufuatia Ziara ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan nchini Kenya ikiwa ni kuitikia mwaliko aliopewa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyata. Ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kwa nchi zote Mbili kwani kuanzia Tarehe 05/05/2021 vikwazo vya Wafanyabiara wa Tanzania kuingiza mahindi nchini Kenya vimeondolewa. Pamoja na mafanikio hayo mambo mengine ya manufaa ni:- Kujenga na kuendeleza utamaduni wa kukutana mara kwa mara, hii itasaidia kutatua changamoto ndogondogo zinazojitokeza. Kushirikiana kwenye sekta ya utalii, kwamba badala ya kunyanganyana watalii busara itatumika kuwashawishi watalii kuongeza siku za kutembelea Kenya na Tanzania. Vyombo vya ulinzi kushirikiana kulinda maeneo yote ili kusaidia kuwepo kwa utulivu na kutoa fursa ya shu

Ujumbe wa Wakili Msomi kwa Wanaharakati wa Kenya

Picha
Kwanza ninaanza kwa kuwasalimia kwa salamu ya jina la Jumuiya ya Afrika Mashariki, poleni na hongereni kwa utekelezaji wa Majukumu yenu ya kila siku. Nimeguswa kuwatumia ujumbe wa wazi kufuatia ujumbe wenu mlioutoa kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu wa kumtaka awaachie huru wafugwa wa Kisiasa. Naelewa ujumbe wenu huu mmeutoa kufuatia Mhe. Rais Samia Suluhu kutoa Msamaha wa wafungwa 5001 siku ya maadhimisho ya miaka 57 ya Muungano wa Tanzania . Mmesema bado kuna wafungwa 200 wako Magereza kwamba mnamjulisha Mhe.Rais kwamba hajui!!!, Mhe. Rais anajua kila kinachoendelea nchini maana yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu, na anauwezo wa kuwaachia huru kama alivyofanya kwa wafungwa 5001, lakini uwezo huo alionao ni kwa mujibu wa sheria za nchi na siyo tu kwa mamlaka aliyonayo kama Rais. Mnapaswa kujua kuwa Wafungwa hao 5001 waliopewa msamaha na Rais kati yao 1516 wameachiwa huru baada ya kupunguziwa robo ya adhabu na Wafungwa 3,485 wamepunguziwa robo ya adhabu bada