TUNDU LISSU ULIKUWA UNATUDANGANYA!!
Na WanaCHADEMA Kanda ya Kaskazini
Yuko wapi Tundu Lissu ambaye alituhamasisha wananchama wa CHADEMA kuandamana nchi nzima kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu, hayupo nchini ameondoka kwenda Ubelgiji huku akisindikizwa na maafisa wa Ubalozi wa Ujerumani mpaka uwanja wa ndege!!!
Hapa ndipo tunapogundua kuwa Tundu Lissu hakuwa pamoja nasi bali alikuwa anatudanganya kwa kutushawishi tuingie barabarani kuandamana na kufanya vurugu ilhali akijua kwa upande wake haitamletea matatizo kwa kuwa alishaandaliwa mpango na Mataifa ya Magharibi kuondolewa nchini baada ya kusababisha vurugu na machafuko nchini.
Sasa tunajiuliza endapo tungeingia barabarani kuandamana tungekuwa katika hali gani? Maana aliyekuwa anahamasisha maandamano angekuwa katika mazingira salama na kutuacha sisi tukiwa katika hali mbaya baada ya kusababisha vurugu nchini, tungekosa mahali pa kwenda, kwani wote walikuwa wanaunga mkono maandamano wameshapata mahali pa kujihifadhi, Tundu Lissu nchini Ubelgiji, Godbless Lema nchini Kenya, na Evarist Chahali nchini Scotland.
Hata hawa wengine akina Freeman Mbowe, Zitto Kabwe, Maria Sarungi na wengineo wana mahali pa kwenda kwani watapewa hifadhi na mabeberu ambao wanawalipa fedha nyingi kwa kuwatumikisha katika masuala kisiasa kwa maslahi ya nchi zao.
Tulikuwa tukisikia tu kuwa Tundu Lissu ni kibaraka wa mabeberu, lakini jana tumeshuhudia kwa macho yetu kuwa kweli ni kibaraka, kwani amesindikizwa na maafisa wa Ubalozi wa Ujerumani mpaka uwanja wa ndege kwa ajili ya safari yake ya kwenda nchini Ubelgiji, kwa taarifa tulizipata ni kwamba amepewa fedha nyingi na kuahidiwa kuwa watamlea hadi atakapokufa.
Tunasosoneka baada ya kugundua kuwa Tundu Lissu pamoja na viongozi wengine wa chama walikuwa wanatudanganya kwa kujifanya wako pamoja nasi kumbe tayari walikuwa wametengenezewa mazingira ya kupata hifadhi katika mataifa ya nje baada ya kushindwa kutimiza azma yao ya kusababisha machafuko nchini.
Tulipumbazwa na maneno ya Lissu na Viongozi wetu wa chama na hata tuliposikia maneno ya watu wakituambia kuwa Tundu Lissu anahamasisha tuandamane kwa sababu anajua baada ya uchaguzi ataondoka nchini na ana tiketi ya ndege ya kuondoka tulikataa na kujidanganya wenyewe kuwa atakwenda tu kwenye matibabu na kurudi, sasa tunapata wakati mgumu kuamini kuwa yaliyokuwa yakisemwa ni ya kweli.
Hata hivyo, tunamshukuru Mungu kwa kuwa hatukuingia barabarani kaundamana kwani tungekuwa tumeingia katika machafuko na kukosa mahali pa kwenda huku viongozi wetu wakiwa katika mazingira salama pamoja na familia zao.
Akili za kuambiwa changanya na za kwako.
Maoni
Chapisha Maoni